A TOWN BOYS ARUSHA

WAJUE KABILA LA WAHADZABE KUTOKA KASKAZINI MWA TANZANIA ARUSHA

 Hadza au Wahadzabe ni kabila linaloishi katika kaskazini ya kati Tanzania wanoishi kuzunguka ziwa Eyasi katikati ya bonde la ufa na eneo la jirani ya serengeti na hapa ni vijana wakicheza ngoma za kitamaduni.
 Hadza ni kabila lenye idadi ya watu wasiozidi 1000 na hapa ni binti wa kabila la hadza akicheza zeze ya kiasili.hii inaonyesha ni jinsi gani muziki siyo teknolojia.
 Wanatofautiana na watu wa kawaida kijenetikia na jadi yao ni ya lugha ya Khoisan inayoonekana kujijenga na kutohusiana na watu wengine
 Baadhi ya mapambo ya kitamaduni na fuvu za wanyama kutokana na kabila hili kuishi kwa kutegemea uwindaji kwa kiasi kikubwa.
 Karibu kuwatemelea Wahadzabe na ujue kuusu utamaduni wao.Tunaweza kuandaa safari za kutembelea makabila mbalimbali kutokana na vile unavyotarajia kujifunza na kukuza utalii wa ndani na nje pia.Karibu Arusha weka maoni yako kwa unachotaka kujua kuusu kuwatembelea.  


Wahadzabe wana maeneo manne ya makazi kame kusini mwa Ziwa Eyasi na kati ya ziwa Eyasi na Bonde la Yaeda mashariki katika nyanda za juu Mbulu( Siponga) na kaskazini mwa bonde karibu na mji wa Mang"ola.


Wakati wa msimu wa mvua Hadzabe hutoka nje  kati ya maeneo haya na usafiri kiurahisi msimu wa kiangazi na hii ni nyumba ya kuishi inayotumika na kabila la Wahadzabe
 Kabila hili linaishi kwa kutegemea uwindaji wa wanyama kwa kiasi kikubwa na chakula chao kikuu ni nyama ambayo huifadhiwa kwa kuanikwa juani kwenye miti.Pichani ni baadhi ya wanyama pori aina ya swala ambao Hadza huwawinda kwa wingi
 Pia wanishi kifamilia na hapa na wakina mama na watoto wa kabila la Hadza.Rika la vijana huwa wanawinda na chakula kuliwa na wote
Matumizi ya tumbaku na bangi na moja ya starehe ya vijna wengi wa kabila la Wahadzabe na kuwasha moto huwa wanatumia kijiti kikavu, magome ya mti kupekecha hadi moto kuwaka na kutumika kwa matumizi mbalimbali na Hadza 300 hadi 400 hishi kwa kiasi kikubwa kwa uwindaji kama babu zao. KARIBU ARUSHA.





Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

6 comments:

  1. Nalipenda sana kabila LA hadzabe Mungu atatusaidia miaka ijayo tutatoa Rais wa Tz

    ReplyDelete
  2. Nalipenda sana kabila LA hadzabe Mungu atatusaidia miaka ijayo tutatoa Rais wa Tz

    ReplyDelete
  3. Je kabila hili hutumia mfumo gani katika kusoma au kuna while zimejengwa katika jamii yao?

    ReplyDelete
  4. Kuna shule zimejengwa kwajili yao?

    ReplyDelete
  5. Je,kabila hili wako Jimbo gani na kiongozi wao ni nani?

    ReplyDelete
  6. Kabila hili Kuna siku niliwahi sikia eti wanakula nyamaa za watu. Je ni kweli a

    ReplyDelete