A TOWN BOYS ARUSHA

KUPUNGUZA MAAMBUKIZI YA VVU.

Jumuiya ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (Muhas), imeboresha hali ya vitendea kazi katika sehemu ambazo ni hatarishi zaidi ili kulinda watendaji wake dhidi ya maambukizi ya vvu yanayoweza kutokana na mazingira ya kazi
Akizungumza katika maadhimisho ya siku ya Ukimwi Duniani juzi, Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Ephata Kaaya, alisema miongoni mwa maeneo yaliyopewa kipaumbele zaidi ni kwenye maabara zote sambamba na ufungaji wa mashine za kutoa kondomu za kiume kwenye mabweni ya wanafunzi 
“Sisi wa Muhimbili kutokana na elimu tunayojifunza au kufundisha sio kweli kwamba tuko kwenye hali bora zaidi ya kuweza kujikinga na ugonjwa wa Ukimwi ni lazima tuchukue tahadhari,” alisema Kaaya.
Alisema zaidi ya asilimia 90 ya maambukizi yote ya vvu nchini yanatokana na kujamiiana, huku asilimia iliyobaki ikiangukia kwenye sababu nyingine za maambukizi
Makamu Mkuu wa chuo hicho alisisitiza kuwa ni wajibu wa kila mmoja kuunganisha nguvu katika kupunguza maambukizi na adha za kuugua Ukimwi kwani madhara yake yanafahamika kuanzia kwenye familia, jumuiya na taifa na hayatofautiani kati ya jamii na jamii au familia na familia
Kaaya alisema hadi sasa dunia imeshapoteza watu takribani milioni 25 tangu kugundulika kwa kirusi cha vvu mwaka 1981, huku wengine wapatao milioni 35 wakiishi na virusi hivyo
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment