A TOWN BOYS ARUSHA

Waishtaki Sumatra kwa Dk Mwakyembe

Dar es Salaam. Chama cha Kutetea Abiria (Chakua) kimemwomba Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe kuingilia kati suala la kuanza kwa matumizi ya mfumo mpya wa ukatishaji tiketi kwa njia ya mtandao kwa mabasi yaendayo mikoani, kwa madai kuwa Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra), imekuwa chanzo cha ucheleweshwaji wa kuanza kutumika kwa mfumo huo.
Akizungumza na waandishi wa habari juzi, mwenyekiti wa Chakua, Hassan Mchanjama alisema wadau wote wakiwamo Wamiliki wa Mabasi (Taboa), Jeshi la Polisi na Kikosi cha Usalama Barabarani, waliridhia kuanza kutumika kwa  mfumo huo unaodhaniwa utasaidia kupunguza kero wanayoipata abiria kutoka kwa wapiga debe, lakini cha kushangaza Sumatra haijachukua hatua ya kutoa agizo kwa wenye mabasi kuanza rasmi kutumia mfumo huo.
Alisema adha wanayoipata sasa abiria ya kupandishiwa nauli kiholela kipindi cha sikukuu na shule zinapofungwa au kufunguliwa pamoja na kulanguliwa tiketi na madalali, lisingekuwapo kama mfumo huo wa ukataji tiketi ungekuwa unatumika.
“Taboa hawana tatizo na mfumo huu, wadau wote tulishakubaliana na katika kikao cha mwisho kilichofanyika Desemba, mwaka jana, Sumatra ilipewa miezi mitatu ya kutathmini ili baadaye itoe tangazo kwa wamiliki wote  wa mabasi kujiunga katika mfumo huo, kitendo ambacho hawajafanya mpaka sasa,” alisema Mchanjama.
Hata hivyo, meneja uhusiano wa Sumatra, David Mziray alipinga madai hayo na kusema wao siyo wahusika wanaosimamia ama  kuidhinisha kampuni itoe  huduma ya aina gani kwa abiria wake.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment